ETETA | Home juu

Ijue ETETA

Zipo sababu nyingi na ambazo zilichangia katika uanzishwaji wa ETETA

Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi 2015-2020

Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imesisitiza Elimu kwa TEHAMA katika kuwezesha walimu na wanafunzi kutumia TEHAMA kufundishia na kujifunzia katika ngazi zote za Elimu. Pia imehimiza mafunzo ya Elimu mtandao na Maktaba mtandao.

Utekelezaji wa Sera ya Elimu ya Tanzania ya Mwaka 2014

Sera ya Elimu Tanzania ya mwaka 2014 imehimiza matumizi ya TEHAMA katika kutoa Elimu vizuri na sitahiki. Pia imesisitiza matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa Elimu na mafunzo katika ngazi zote za Elimu.

Utekelezaji Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa 2015-2030

Lengo la tisa la mpango wa maendeleo wa Umoja wa Mataifa, linalenga kukuza uelewa wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika kusaidia kushughulikia changamoto kubwa za duniani kama vile kujenga ajira na kuwa na nguvu zaidi ya Nishati na Matumizi bora ya mawasiliano ya Mtandao

Kuongeza Idadi ya Watumiai wa TEHAMA Tanzania

Kutokana na Takwimu za Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia mitandao na Matumizi ya TEHAMA (ICT Index), kwenye ripoti yake ya mwaka 2017 inaonyesha kuwa nchi ya Tanzania ni ya 164 kati ya nchi 169 Duniani katika matumizi ya TEHEMA. Hii inaonyesha tunahitataji kuongeza idadi ya watumiaji wa TEHAMA katika Shughuli za Kila Siku za kuleta Maendeleo.

Utekelezaji Mpango Mkakati wa Mkoa Morogoro

Mkoa Morogoro umelenga kutoa Elimu kwa TEHAMA, njia hii itasaidia kupata wataalamu mahiri watakaosaidia kupatikana kwa wataalamu wengine watakaoweza kutumia rasilimali zilizopo.

Mpango mkakati wa Seksheni ya Elimu Mkoa wa Morogoro

Sekisheni ya Elimu katika Mkoa wa Morogoro iliazimia walimu na wanafunzi wawe na uwezo wa kutumia Vifaa vya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji ili kuboresha Elimu ifikapo 2022 na kuufanya Mkoa uwe wa Kidijitali.

Wahisani

  • Wahisani
  • Wahisani
  • Wahisani
  • Wahisani
  • Wahisani